SiasaMali
Mali yawakamata wanajeshi kwa tuhuma za usaliti
11 Agosti 2025Matangazo
Hayo yameelezwa jana na shirika la habari la AFP likinukuu vyanzo kadhaa vilivyosema kuwa karibu askari 50 wametiwa nguvuni. Miongoni mwa waliokamatwa ni Jenerali Abass Dembele, Gavana wa zamani wa Jimbo la Mopti na afisa wa kijeshi anayeheshimika.
Tangu ulipoingia madarakani mwaka 2021, utawala wa kijeshi katika nchi hiyo ya Magharibi mwa Afrika umezidisha ukandamizaji kwa wale wote wanaokosoa machafuko makubwa yanayosababishwa na operesheni za kukabiliana na makundi ya itikadi kali yanayopatikana katika kanda ya Sahel.