JamiiVatican
Makadinali kuanza kujiandaa huko Vatican kumchagua Papa Mpya
6 Mei 2025Matangazo
Kufuatia kifo cha Papa Francis mnamo Aprili 21, makadinali 133 watakaopiga kura hiyo watakusanyika kesho Jumatano katika Kanisa dogo la Sixtine ili kumchagua miongoni mwao Papa mpya atakayewaongoza Wakatoliki wapatao bilioni 1.4 duniani.
Kongamano hilo la kipekee litakalowajumuisha wawakilishi kutoka nchi 70 linachukuliwa kuwa kubwa zaidi na la kimataifa kuwahi kushuhudiwa katika historia ya Kanisa hilo lenye ushawishi mkubwa duniani kote, lakini linalotaabika kuendana na ulimwengu wa kisasa na kurejesha haiba yake baada ya kashfa ya kuenea kwa vitendo vya unyanyasaji wa kingono kwa watoto vilivyofanywa na makasisi.