MigogoroUlaya
Makabaliano ya Urusi na Ukraine yasababisha vifo na majeruhi
31 Mei 2025Matangazo
Maafisa kwenye mikoa miwili ya Ukraine ya Kherson na Zaporizhzhya wameripoti kifo kimoja kwa kila eneo kutokana na mashambulizi ya Urusi.
Moscow nayo imesema watu 14 wamejeruhiwa kwenye mkoa wake wa kusini wa Kursk kutokana na mashambulizi ya droni za Ukraine.
Katika hatua nyingine Urusi imetangaza kuvikamata vijiji viwili vya Ukraine, kimoja kwenye jimbo la Donetsk na kingine katika mkoa wa Sumy.
Ukraine imesema imeamuru kuhamishwa kwa watu kutoka vijiji 11 vya mkoa wa mpakani wa Sumy kutokana na mashambulizi ya Urusi.