UgaidiNigeria
Majambazi wawateka watu 60 Kaskazini Magharibi mwa Nigeria
6 Agosti 2025Matangazo
Hayo yameelezwa na mashuhuda wa tukio hilo ambalo ni la pili kutokea kwenye eneo hilo ndani ya siku chache ambapo watu wengine 70 walitekwa siku ya Jumamosi huko Sabongarin Damri, katika jimbo la Zamfara.
Shehu Musa, kiongozi wa jadi huko Damri, ameliambia shirika la habari la Reuters jana jioni kwamba baada ya tukio la Jumamosi, washambuliaji walirejea kwenye eneo hilo Jumatatu na walivamia vijiji vya Sade, Tungar Tsalle, Tungar Sodangi na Tungar Musa Dogo.
Katika miaka ya hivi karibuni, serikali ya Nigeria imekuwa ikipambana na makundi yenye silaha na yale ya itikadi kali ambayo yamewaua mamia ya watu na kuwateka nyara maelfu wengine katika eneo la kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.