BiasharaMarekani
China na Marekani zajadili kupunguza mivutano ya kibiashara
29 Julai 2025Matangazo
Wachambuzi wanatarajia kuwa mazungumzo hayo huenda yakasababisha kuongezwa kwa viwango vya sasa vya ushuru wa bidhaa kati ya mataifa hayo.
Marekani imekuwa ikifanya makubaliano na washirika wake wa kibiashara kuhusu ushuru wakiwemo Umoja wa Ulaya, Uingereza, Japan na Umoja wa Ulaya tangu Rais Donald Trump alipotangaza kuziongezea ushuru nchi kadhaa mwezi Aprili.
Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Bessent na Naibu wa Waziri Mkuu wa China He Lifeng wanashiriki majadiliano hayo japo hawajazungumzia lolote kuhusu yaliyojadiliwa Jumatatu katika siku ya kwanza ya mazungumzo.