JamiiZambia
Mahakama yaagiza mwili wa Lungu kurudishwa nyumbani kuzikwa
8 Agosti 2025Matangazo
Mchana wa Ijumaa, jaji wa mahakama kuu mjini Pretoria alisema mwili wa Lungu unapaswa kukabidhiwa kwa mwakilishi wa mahakama ya Zambia kwa ajili ya kurudishwa nyumbani.
Uamuzi huu unaoegemea upande wa serikali ya Zambia, unatofautiana na familia yake iliyotaka kumzika Afrika Kusini, bila ya uwepo wa Rais wa sasa Hakainde Hichilema, ambaye ni mpinzani wa muda mrefu wa kisiasa wa Lungu.
Lungu, alikuwa rais wa Zambia kati ya mwaka 2015 hadi 2021, na alifariki dunia nchini Afrika Kusini Juni 5 wakati akipatiwa matibabu.