Mahakama ya Uturuki yamhukumu meya wa Istanbul
16 Julai 2025Mahakama hiyo nchini Uturuki imemhukumu Imamoglu kifungo cha mwaka mmoja na miezi minane jela.
Hata hivyo mahakama hiyo ilimuondolea shtaka la kumtambulisha Gurlek hadharani kwa lengo la kumfanya mlengwa.
Imamoglu amekanusha madai hayo.
Mameya watatu wa vyama vya upinzani Uturuki wakamatwa
Meya huyo alikamatwa pamoja na wanasiasa wengine kutoka chama kikuu cha upinzani kama sehemu ya uchunguzi wa tuhuma za rushwa.
Kukamatwa kwake kulisababisha maandamano makubwa zaidi ya mitaani nchini Uturuki katika kipindi cha zaidi ya muongo mmoja.
Uturuki yawakamata wapinzani wa Erdogan Izmir
Imamoglu, ambaye anazuiliwa katika gereza moja magharibi mwa Istanbul tangu Machi 23, anatarajiwa kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo, ambayo ni sehemu ya kesi kadhaa zinazoendelea dhidi yake.