SiasaKorea Kusini
Mahakama ya Seoul yaamuru rais Yoon kuachiwa huru
8 Machi 2025Matangazo
Mahakama ya Wilaya ya Kati ya mjini Seoul imesema uamuzi wake umetokana na kucheleweshwa kwa mashitaka na kumalizika kwa muda wa kuwekwa kizuizini huku ikihoji kuhusu uhalali wa mchakato wa kukamatwa kiongozi huyo.
Soma pia: Mahakama ya Korea Kusini yakataa Rais Yoon kuachiwa huru
Hata hivyo rais huyo amesalia rumande huku upande wa mashtaka ukieleza nia ya kukata rufaa kuupinga uamuzi huo.
Hii ikizingatia kuwa Yoon bado anakabiliwa na mashtaka ya jinai kutokana na uamuzi wake wa kutangaza sheria ya kijeshi iliyoibua mzozo wa kisiasa nchini humo.