Sara Duterte anusurika njama ya kumuondoa madarakani
25 Julai 2025Bunge la Ufilipino lilimuondoa madarakani Duterte mwezi Februari kwa madai ya kutumia vibaya fedha za umma, kujilimbikizia utajiri mkubwa na kutoa vitisho vya kumuua rais wa Ufilipino Ferdinand Marcos Jr, mke wake na spika wa bunge.
Hata hivyo Mahakama hiyo imesema haimuondolei mashtaka Sara Durtete kwa makosa anayokabiliwa nayo.
Uamuzi wa mahakama hiyo unaweza kumnufaisha Bi. Duterte kisiasa.
Rais wa zamani wa Ufilipino Rodrigo Duterte akamatwa kwa warranti wa ICC
Anaonekana kama mgombea shupavu wa urais katika uchaguzi wa mwaka 2028, ambao rais wa sasa Macros hawezi kushiriki kufuatia udhibiti wa mihula. Nchini Ufilipino rais anapaswa kuhudumu kwa muhula mmoja tu.
Sara Durtetet ni mtoto wa rais wa zamani wa Ufilipino Rodrigo Duterte, anayezuiiliwa katika mahakama ya ICC kufuatia mashitaka ya uhalifu dhidi ya ubinaadamu kuhusiana na vita vyake vya umwagaji damu dhidi ya dawa za kulevya.