Mahakama ya ICC yaahirisha kesi ya Duterte
9 Septemba 2025Matangazo
Dutretealipangiwa afike katika mahakama ya ICC mnamo Septemba 23 kusikiliza mashitaka kuhusu kampeni yake ya miaka kadhaa dhidi ya watumiaji na walanguzi wa dawa za kulevya ambayo mashirika ya kutetea haki za binadamu yanasema iliwaua maalfu.
Lakini mahakama imeamua kuahirisha mpaka itakapoamua kuhusu hoja ya utetezi kwamba kiongozi huyo mzee mwenye umri wa miaka 80 hayuko katika hali nzuri kiafya kuweza kujibu mashitaka na hafai kushtakiwa. Jopo la majaji watatu limegawanyika kuhusu uamuzi huo huku jaji mmoja akipinga.