Maelfu ya watu waandamana Uholanzi dhidi ya Israel
15 Juni 2025Matangazo
Makundi ya kutetea haki kama vile Amnesty International na Oxfam yaliandaa maandamano hayo kupitia mji huo hadi Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ.
Wengi wakipeperusha bendera za Palestina na wengine wakiimba "Komesha Mauaji ya Kimbari", waandamanaji hao waligeuza bustani moja kuu mjini humo kuwa eneo jekundu .
Umoja wa Mataifa wapiga kura kutaka usitishaji mapigano Gaza
Waandamanaji pia walibandika mabango yaliyokuwa yameandikwa "Usiangalie kando, fanya kitu", "Acha ushirika wa Uholanzi", na "Nyamaza watoto wanapolala, sio wanapokufa".
Waandaji waliitaka serikali ya Uholanzi iliyosambaratika Juni 3 baada ya chama cha mrengo mkali wa kulia kujiondoa katika muungano dhaifu kuchukuwa hatua zaidi kuidhibitiIsraeli.