Macron ataka kubuniwa kwa miungano mipya ya kikanda
30 Mei 2025Matangazo
Akizungumza wakati wa mjadala wa Shangri-La huko Singapore, Macron amesisitiza haja ya kuunda miungano mipya kati ya Ufaransa na washirika wake wa eneo la Indo-Pasifiki.
Macron amesema mabara ya Asia na Ulaya yana mtazamo mmoja katika kuzuia kusambaratika kwa mfumo wa dunia.
Macron anafanya ziara barani Asia wakati Ufaransa na Umoja wa Ulaya zinalenga kuimarisha mahusiano ya kibiashara barani humo, ili kuondoa hali ya wasiwasi inayotokana na ushuru unaowekwa na Rais Donald Trump kwa mataifa ya dunia.