SiasaUfaransa
Macron: Ufaransa haitaki kuchochea "Vita vya Tatu vya Dunia"
14 Mei 2025Matangazo
Katika mahojiano ya televisheni yaliyodumu kwa zaidi ya saa tatu, Macron ameahidi kuandaa kura ya maoni kuhusu masuala muhimu wakati akieleza malengo yake kwa kipindi kilichosalia cha miaka miwili ya muhula wake madarakani.
Kiongozi huyo aliyeingia madarakani mwaka 2017 akiahidi mabadiliko makubwa, atamaliza muda wake mwaka 2027 baada ya kuhudumu kwa mihula miwili inayoruhusiwa na katiba.
Soma pia: Urusi yakataa kupangiwa na EU kusitisha vita Ukraine
Katika miezi ya hivi karibuni, Macron ameonekana kuchukua jukumu kubwa la kujaribu kuvimaliza vita vya miaka mitatu kati ya Urusi na Ukraine.
Ameyahimiza mataifa ya Ulaya kuisaidia Ukraine kujilinda japo kwa tahadhari bila ya kuchochea Vita vya Tatu vya Dunia.