SiasaMarekani
Maafisa wa Urusi na Marekani wakutana mjini Istanbul
10 Aprili 2025Matangazo
Shirika la habari la AFP, limeripoti kuwa wajumbe wa Urusi na Marekani wamewasili katika jengo la ubalozi mdogo wa Urusi mjini Istanbul.
Siku ya Jumanne, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani Tammy Bruce, aliwaambia waandishi habari kwamba pande hizo mbili zitajaribu kuimarisha zaidi shughuli za balozi hizo mbili.
Ukraine haiko katika ajenda ya mazungumzo
Bruce amesema hakuna masuala ya kisiasa au usalama kwenye ajenda na Ukraine haitajadiliwa kabisa.
Mazungumzo hayo ambayo ni ya pili ya aina yake, yanafanyika baada ya Rais Donald Trump kuwasiliana naUrusiwakati alipoanza muhula wake wa pili madarakani, na kuahidi uhusiano bora zaidi ikiwa Urusi itamaliza mapigano yake nchini Ukraine.