M23 yaingia katika mji wa Walikale mashariki mwa Kongo
20 Machi 2025Milio ya risasi ilisikika usiku wa jana karibu na mji huo katika eneo la Nyabangi ambako mapigano yamekuwa yakiendelea kati ya waasi wa M23 na jeshi la Kongo katika mji huo wa Walikale wenye utajiri mkubwa wa madini unaopatikana takriban kilometa 125 kaskazini magharibi mwa Goma.
Hayo yakiarifiwa, rais wa Kongo Felix Tshisekedi amesema nchi yake inatarajia kuimarisha uwezo wake wa ulinzi na usalama kama sehemu ya mkataba wa ushirikiano na Marekani, ambapo Washington itanufaika pia na madini ya Kongo.
Katika hatua nyingine, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron aliwapokea jana wawakilishi wa makanisa ya Kongo ambao wanajaribu kurejesha amani mashariki mwa nchi hiyo. Macron amesisitiza kuwa anaunga mkono mchakato wa mazungumzo ili kuutafutia suluhu mzozo huo wa mashariki mwa Kongo.